Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Cereals and Other Produce Regulatory Authority

(COPRA)

COPRA Logo
"Commercialization of the Tanzania’s Food systems to catalyze growth and resilience"

TANZANIA IMESHIKA NAFASI YA PILI DUNIANI KWA UZALISHAJI WA MBAAZI

Reason Image

Tanzania imeshika nafasi ya pili duniani kwa uzalishaji wa Mbaazi ambapo kwa msimu wa mwaka jana  imesafirisha takriban tani 350,000 kwenda nchini India. Katika Msimu wa Mwaka huu  mbaazi zinazozalishwa Tanzania zinatarajiwa  kuwa zaidi ya  tani 400,000. Kutokana na ongezeko la uzalishaji kumepelekea kushuka kwa bei ya mbaazi duniani. Katika kuwawezesha  wakulima wa zao hilo kupata soko,  Serikali ya Tanzania inachukua hatua za makusudi za kufanya Mpango wa kuuza Mbaazi moja kwa moja kwenda Serikali ya India.

Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA), imeongoza ujumbe wa serikali kwenda nchini India kuendeleza mazungumzo ambapo wamekutana na Katibu Mkuu wa Wizara inayosimamia masuala ya walaji  na kuongelea Mpango  huo wa Tanzania na utekelezaji wake.