Waziri wa Kilimo Mhe. Daniel Chongolo (Mb) akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) inayoonesha aina ya mazao yanayosimamiwa na mamlaka hiyo kwenye kikao kazi cha waziri na viongozi wa taasisi zilizo chini ya wizara hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) Bi. Irene M. Mlola akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Mamlaka hiyo wakati wa Mkutano wa Mwaka wa Watumishi uliofanyika kuanzia tarehe 13 - 15 Novemba 2025 kwenye ukumbi wa Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere uliopo Kibaha mkoani Pwani. Mkutano huo uliwakutanisha watumishi wote wa COPRA makao makuu na ofisi za kanda zote ikijumuisha watumishi wenye ajira za kudumu, watumishi wa mkataba na watumishi wanaopatiwa elimu kwa vitendo. Pamoja na kujadili masuala ya kiutumishi, mkutano huo umetumika kufahamiana miongoni mwa watumishi kwa kushiriki pamoja mazoezi ya utimamu wa mwili, michezo ya kuimarisha timu na birudani.
Katika Picha : Kaimu Mkuu wa Sehemu ya Mazao ya Bustani Bi. Lilian Mpinga akiwa kwenye picha ya pamoja na vijana 50 wanaopatiwa mafunzo elekezi ili kuongeza uzalishaji katka zao parachichi. Mafunzo yamefanyika katika Ukumbi wa Royal Palm uliopo Mkoani Iringa kuanzia tarehe 10 - 12, Novemba 2025
SALAMU ZA PONGEZI KUTOKA KWA BODI YA WAKURUGENZI, MENEJIMENTI NA WAFANYAKAZI WA COPRA
SALAMU ZA PONGEZI KUTOKA KWA BODI YA WAKURUGENZI, MENEJIMENTI NA WAFANYAKAZI WA COPRA
Uzinduzi wa Mpango wa Kitaifa wa Utoaji wa Mbegu za Mbaazi, Ufuta, Choroko, Dengu na Soya katika Mkoa wa Shinyanga tarehe 23 Oktoba 2025
Leo tarehe 9 Julai, COPRA imesaini makubaliano ya kimkakati na Yas Business pamoja na MIXX by Yas, kwa lengo la kuimarisha matumizi ya mifumo ya kidigitali katika upatikanaji wa masoko, taarifa sahihi za bei ya mazao, malipo, na huduma nyingine za kifedha kwa wakulima na wadau katika mnyororo wa thamani wa mazao ya nafaka na mazao mchanganyiko.
Makubaliano haya ni sehemu ya jitihada za COPRA za kukuza uwazi wa soko, kuongeza ufanisi katika biashara ya mazao, na kuwezesha wakulima kupata huduma kwa njia ya haraka na salama kupitia teknolojia.
Tanzania imeshika nafasi ya pili duniani kwa uzalishaji wa Mbaazi ambapo kwa msimu wa mwaka jana imesafirisha takriban tani 350,000 kwenda nchini India. Katika Msimu wa Mwaka huu mbaazi zinazozalishwa Tanzania zinatarajiwa kuwa zaidi ya tani 400,000. Kutokana na ongezeko la uzalishaji kumepelekea kushuka kwa bei ya mbaazi duniani. Katika kuwawezesha wakulima wa zao hilo kupata soko, Serikali ya Tanzania inachukua hatua za makusudi za kufanya Mpango wa kuuza Mbaazi moja kwa moja kwenda Serikali ya India. Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA), imeongoza ujumbe wa serikali kwenda nchini India kuendeleza mazungumzo ambapo wamekutana na Katibu Mkuu wa Wizara inayosimamia masuala ya walaji na kuongelea Mpango huo wa Tanzania na utekelezaji wake.
Leo tarehe 26/08/2025, Watumishi wa COPRA – Nyanda za Juu Kusini wametembelea taasisi za kilimo ikiwemo TPHPA, TFRA na SAGCOT. Lengo la ziara hii lilikuwa kufahamiana, kubadilishana mawazo na uzoefu baina ya taasisi husika, pamoja na kujadili namna bora ya kushirikiana katika utekelezaji wa shughuli za pamoja (joint activities) kwa manufaa ya sekta ya kilimo.
Balozi wa India nchini Tanzania Mhe. Bishwadip Dey amekutana ametembelea Banda la Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA), katika maonesho ya Kimataifa ya Kilimo 2025 yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma.
Tukutane Nane Nane 2025: Tembelea Banda la COPRA katika Ofisi za Kanda zilizopo nchini. “Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi 2025“
Leo tarehe 9 Julai, COPRA imesaini makubaliano ya kimkakati na Yas Business pamoja na MIXX by Yas, kwa lengo la kuimarisha matumizi ya mifumo ya kidigitali katika upatikanaji wa masoko, taarifa sahihi za bei ya mazao, malipo, na huduma nyingine za kifedha kwa wakulima na wadau katika mnyororo wa thamani wa mazao ya nafaka na mazao mchanganyiko.
Miongoni mwa viongozi waliotembelea banda la COPRA leo tarehe 7 Julai 2025 ni Mrajisi wa Vyama vya Ushirika Dkt. Benson Ndiege. Viongozi mbalimbali na wanachi wanaendelea wametembelea banda la Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) katika Maonesho ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba).
Rais mstaafu wa awamu ya nne, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, alipotembelea banda la COPRA akiwa ameambatana na Mhe. Waziri wa Viwanda na Biashara, Suleiman Jaffo, katika kuadhimisha sherehe za Sabasaba Jijini Dar es Salaam mwaka 2025.
Tarehe 13 Novemba, Mkurugenzi Mkuu wa COPRA, Irene Madeje Mlola, alishiriki katika kikao kuhusu “Sera za Biashara na Uwekezaji ili Kukuza Mipango ya Hali ya Hewa na Maendeleo Endelevu” katika Mkutano wa COP 29.